08 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Wananchi waliokuwa wakiishi karibu na mlima Oldonyo Lengai warejea katika makazi yao
 
2008-05-08 14:36:59
Na Radio One Habari

Wananchi waliokuwa wakiishi karibu na mlima Oldonyo Lengai wilayani Ngorongoro ambao waliyakimbia makazi yao kutokana na kulipuka kwa volcano katika mlima huo, wameanza kurejea katika makazi yao.

Hali hiyo imetokana na kutoweka kwa uwezekano wa volcano hiyo kulipuka tena.

Wakizungumzia uamuzi wao wa kurudi tena karibu na mlima huo wananchi hao wamesema maelezo yanayotolewa na serikali na wataalam wake ya kuwataka kukaa mbali na mlima huo hayajitoshelezi na kwamba hayalingani na hali halisi.

Hata hivyo, Mkuu wa wilaya Ngorongoro Bwana Jowika Kasunga amekanusha uvumi ulioenea kwa wananchi hao kuwa nia hiyo ya serikali ni njama za kutaka kuwapora wananchi ardhi yao na kuwapa wawekezaji.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.