09 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Wakazi wa Rufiji walipwa fidia kwa mradi wa umeme wa Songas
 
2008-05-09 16:41:53
Na Radio One Habari

Wakazi wa vijiji viwili vya wilaya ya Rufiji wamelipwa fidia ya mazao na baadhi ya nyumba zao zilizobomolewa ili kupisha mradi wa umeme wa Songas kutoka Songosongo mkoani Lindi.

Wakizungumza na Radio One Stereo wakazi wa vijiji vya Umwe Kaskazini na Mkupuka wameishukuru serikali kwa kuwapatia haki yao.

Akizungumzia suala hilo, Afisa Ardhi wa wilaya ya Rufiji Bwana Leo Rwegasira amesema shilingi milioni 153 zimetolewa na serikali kwa ajili ya kulipa fidia hizo.

Bwana Rwegasira amesema kuwa mpaka sasa kwamba vijiji 14 kati ya 16 tayari vimelipwa na ametoa wito kwa wakazi hao kuwapa ushirikiano wafanyakazi wa mradi huo ili uweze kukamilika mapema.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.