|
Akinamama wa jijini Mwanza waomba biashara zao ndogondogo kurasmishwa
2008-05-15 17:29:02
Na Radio One Habari
Baadhi ya akina mama wanaofanya biashara ndogo ndogo jijini Mwanza wameoimba serikali kutambua na kurasmisha biashara wanazofanya ili kuondokana na usumbufu na hasara wanazopata kutokana na misako ya mara kwa mara ya mgambo wa halmashauri ya jiji hilo.
Wakiongea na Redio One Stereo akina mama hao wamesema wanawake ndio walezi wa familia kutokana na ama kufiwa au kukimbiwa na waume kutokana na hali ngumu ya maisha.
Aidha wameiomba serikali na taasisi za fedha kuwapa mikopo yenye masharti nafuu ili kuinua mitaji yao.
|