|
Kilosa waomba kuianishiwa mipaka ya wakulima na wafugaji
2008-05-15 17:35:54
Na Radio One Habari
Wakazi wa wilaya ya Kilosa wameiomba serikali kuainisha mipaka ya ardhi kwa wakulima na wafugaji, ili kuepusha migogoro kati ya makundi hayo.
Wakizungumza na Radio One Sterio wamesema katika baadhi ya vijiji mipaka imefutika hali ambayo inachangia migogoro kati ya wakulima na wafugaji .
Aidha wamelalamika kuwa baadhi ya wafugaji hulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima kutokana na kukosekana kwa maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo.
Wamesema kama serikali haitaweka mipaka huenda yakazuka mapigano baina ya wakulima na wafugaji na wameiomba serikali kutoa elimu ya sheria ya umiliki wa ardhi kwa wakulima na wafugaji wa wilaya hiyo ya Kilosa ili kuepusha migogoroya ardhi isiyokuwa ya lazima.
|