16 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Kundi kubwa la tembo limevamia mashamba na kufanya uharibu
 
2008-05-16 15:47:43
Na Radio One Habari

Kundi kubwa la tembo kutoka katika pori la hifadhi la Maswa limevamia mashamba na kuharibu hekta 90 za mazao mbalimbali ya wananchi katika wilaya ya Meatu mkoani Shinyanga katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Akitoa taarifa ya wilaya hiyo kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Ezekiel Maige, Mkuu wa wilaya ya Meatu Bwana Abihudi Saideya amesema tembo hao walivamia mashamba hayo kati Aprili mwaka jana na Aprili mwaka huu katika vijiji sita vya wilaya hiyo.

Bwana Saideya amesema tembo hao waliharibu mazao ikiwemo mahindi, viazi, miwa, mboga na matunda ambapo hasara iliyosababishwa na uharibifu huo bado haijafahamika na kwamba wananchi walioathirika watakabiliwa na uhaba wa chakula mwishoni mwa mwaka huu.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Maige ameuagiza uongozi wa wilaya hiyo kuendelea kutoa elimu ya kuwataka wananchi kuacha kulima karibu na hifadhi hiyo.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.