|
Toto washauri
2008-05-04 09:29:22
By Mwandishi Wetu
Baada ya kunusurika kushuka kwenye ligi kuu ya Bara, timu iliyopanda daraja mwaka jana ya Toto African imelishauri shirikisho la soka, TFF, kutumia wachezaji wa zamani kama waamuzi ili kupunguza maamuzi mabaya.
Kocha mkuu wa Toto Charles Kilinda alisema mapema wiki hii waamuzi wengi wamechezesha mpira vibaya msimu huu kutokana na wenyewe kutocheza soka kabla.
Kilinda alisema waamuzi wengi waliochezesha mechi za timu yake hawakutoa maamuzi ya haki, walikuwa wenye jazba na hasira na wengine walionyesha dhahiri kutojua wakifanyacho.
``Nilidhani wachezaji wa zamani waliocheza soka ndio wenye kustahili kuwa waamuzi kwani wao soka wanalijua kwa kuwa wamelicheza na hawawezi kutafsiri sheria kutoka kwenye vitabu,`` alisema Kilinda.
|