Hatua stahiki zichukuliwe katika kukabiliana na vitendo hivi viovu
TANZANIA imekuwa ikichukua tahadhari mbalimbali dhidi ya matishio yanayoweza kujitokeza yakiwamo ya ugaidi hasa kutokana na kuwapo kwa vikundi vinavyojihusisha na vitendo hivyo katika nchi jirani. Miongoni mwa hatua hizo ni kutungwa kwa Sheria ya Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2022 ambayo msukumo mkubwa ulitokana hasa na uvamizi wa ofisi za ubalozi Dar es Salaam na Nairobi, Kenya mwaka 1998.