ACT Wazalendo wapiga jeki ujenzi wa kanisa, kiongozi wa chama atoa mil. 1/-

By Sabato Kasika , Nipashe
Published at 03:41 PM Jul 22 2024
Dorothy Semu akizungumza katika harambee hiyo.
Picha: Mpigapicha Wetu
Dorothy Semu akizungumza katika harambee hiyo.

KIONGOZI wa Chama Cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amechangia Sh. milioni 1.1, kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), mtaa wa Ihami usharika wa Ikwete, Jimbo la Makambako mkoani Njombe.

Wakati akichangia kiasi hicho cha fedha, viongozi wengine wa chama hicho, Mwenyekiti wa chama Masoud Othman Masoud aliyeahidi kuchangia Sh. milioni mbili, Kiongozi wa mstaafu Zitto Kabwe Sh. milioni moja na katibu mkuu Ado Shaibu Sh.milioni moja.

Dorothy ambaye alikuwa mgeni rasmi, alichangia fedha hizo juzi, wakati akiendesha harambee ya kuchangia Sh. milioni 13,360,000 zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.

KIONGOZI wa Chama Cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu, akiteta jambo na Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kusini.

Katika harambee hiyo, michango kutoka kwa waumini waliokuwapo katika tukio hilo, ilikuwa ni fedha taslimu Sh. 1.3, huku ahadi ikiwa ni shilingi 60,000.

Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kusini, Grayson Shilongoji, ameshukuru ushiriki wao,  katika harambe hiyo na kuwaomba waendelee na moyo huo kuchangia ujenzi wa nyumba za ibada.

"Kiasi cha fedha tunachotafuta ni Sh. milioni 13,360,000, lakini mwanzo huu si haba, ila ninawaombea muendelee na moyo huo wa kusaidia ujenzi wa nyumba za ibada," amesema  Shilongoji

Waumini wakiwa kwenye eneo la tukio.