Prof. Janabi, kumrithi Dk. Ndugulile WHO

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 01:40 PM Dec 10 2024
Prof. Janabi, kumrithi Dk. Ndugulile WHO

Rais Samia Suluhu Hassan amemshauri Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, kujiandaa kuchukua nafasi ya kimataifa iliyoachwa wazi na Dk. Faustine Ndugulile, aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, kabla ya kufariki dunia Novemba 27,2024.