Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma (PSSSF ), Fortunatus Magambo, alibainisha hayo kwa wahariri kutoka vyombo vya habari waliofanya ziara ya kutembelea na kujionea maendeleo ya mradi wa machinjio ya kisasa.
Alisema mradi huo wa machinjio hayo unamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali kupitia Mfuko wa PSSSF , Eclipse Investiment (LLC) na Kampuni ya Busara Investiment (LLP).
Alisema mradi huo ulianza mwaka 2018, lakini ugonjwa wa Covid -19 ulipoanza ulisababisha mashine zilizoagizwa kutoka nje kuchelewa kuletwa pamoja na wataalamu wake hadi Julai mwaka jana zilipoletwa na kuanza kufungwa na kwamba kazi hiyo ipo kwenye hatua ya mwisho.
Naye Meneja Uhusiano na Elimu kwa wanachama PSSF, James Mlowe, alivitaka vyombo vya habari kuunganisha jamii, Serikali na wadau wa maendeleo katika utoaji wa taarifa sahihi katika uhamasishaji wa kukuza uchumi na maendeleo ya watu.
Mlowe alisema kuwa mfumo wa PSSF umewekeza katika kiwanda hicho wa asilimia 30,ikiwa ni sehemu ya mkakati wake katika uwekezaji wa miradi mbalimbali hasa katika kipindi hiki ambacho taifa limejiwekeza katika uchumi wa viwanda.
“Vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuunganisha jamii,serikali na wadau katika kuhabarisha umma hasa wanachama wa PSSF ili watambue uwezekaji unaofanyika na michango yao ipo salama katika uwekezaji wenye tija” alisema Mlowe.
Nae Mhandisi wa Kiwanda cha nyama cha Nguru, Zuberi Makazini, alisema mabwawa ya kutibu maji taka kiwandani hapo malighafi zake zinazotumika ni za kisasa na hukithi vigezo vya kimataifa.