Akizungumza jana wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau kujadili rasimu ya miongozo ya usalama wa mazingira na jamii katika utekelezaji wa mradi wa kuboresha elimu ya juu ya mabadiliko ya kiuchumi (HEET) kwa wanufaika wa moja kwa moja wa taasisi za serikali, Katibu Mkuu, Dk. Leonard Akwilapo, alisema mradi huo ni muhimu kwa kuwa utaleta mabadiliko makubwa ya kitaaluma nchini.
Alisema kikao kingine cha wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali kitafanyika leo lengo ni kupata maoni ya wadau katika maboresha na utekelezaji wa miradi huo na wanataaluma, na kesho kutakuwa na kikao cha wadau wengine.
Kwa mujibu wa Dk. Akwilapo, mradi huo unakuja kujibu changamoto za elimu zilizopo nchini na kuishukuru WB kwa kufadhili mradi unaotambua mahitaji ya nchi katika sekta ya elimu.
Soma zaidi: https://epaper.ippmedia.com