Dk Michael ameyasema hayo leo jijini hapa mara baada ya kuwasili katika Ofisi yake mpya kufuatia mabadiliko madogo yaliyofanyika na Rais Samia Suluhu Hassan.
Amesema atatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia mipango na mikakati ya wizara, maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu ikiwamo mapitio ya mitaala.
Katibu huyo amesema atawasiliana na Ofisi ya Rais, Utumishi ili kujua maeneo yenye uhitaji mkubwa wa watumishi ili mabadiliko ya mitaala yazingatie eneo hilo ili kuwa na wataalam wanaokidhi mahitaji ya serikali.