Miongoni mwa mambo ambayo hawakuyatekeleza ni pamoja na kutambua viashiria vya magonjwa yanayosumbua wanawake ikiwemo saratani ya shingo ya kizazi na kudhibiti wajawazito kujifungulia majumbani.
Wakizungumzia changamoto hiyo baadhi ya watendaji wa sekta hiyo ngazi ya wilaya wakiwemo waganga wakuu wamesema uhaba wa vitendea kazi, wataalam na ugumu wa Jiografia ya maeneo wanayofanyia kazi ni miongoni mwa vikwazo katika utekelezaji wa majukumu yao.