Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Hassan Mwinyikondo akiambatana na Mkurugenzi na Kamati ya Elimu, Afya na Maji wametembelea shule hiyo na kuona athari iliyotokea.
Akiwa katika eneo hilo Mwinyikondo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ramadhani Posi kuhakikisha Mhandisi anafika mapema kufanya tathmini ili wanafunzi waendelee kutumia vyumba hivyo.
Mkurugenzi Posi amesema kupitia mapato ya ndani wamekuwa wakitenga fedha kwa ajili ya sekta ya elimu hivyo kufuatia maafa hayo wataalamu watafika kufanya tathmini na ukarabati utafanyika mapema.
Kuhusu nyumba zilizoezuliwa amesema watajadiliana na Baraza la Madiwani kuona ni mahitaji gani wanaweza kusaidia.
Afisa Elmu Msingi Miriam Kihiyo amesema kwasasa wanafunzi wa shule ya makombe wanasoma kwa awamu katika kipindi hiki ambacho wanasubiri vyumba hivyo kukarabatiwa.
Diwani wa Lugoba Rehema Mwene amesema wananchi ambao nyumba zao zimeezuliwa wamehifadhiwa kwa majirani.