Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba, amezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie kwa kuwekeza na kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.
Kampuni zilizopigwa faini ni pamoja na Airtel iliyotakiwa kulipa faini ya bilioni 11.5, Tigo sh bilioni 13, Halotel sh bilioni 3.4, Vodacom sh bilioni 7.8, Zantel sh bilioni 1 na TTCL sh bilioni 1.3.
“TCRA imeazimia kwamba badala ya kulipwa fedha hizo, tuzielekeze kwa watoa huduma, hivyo kila mtoa huduma atumie kiasi chake alichotakiwa kulipa, akiwekeze katika kuboresha huduma.” amesema Kilaba.
Kilaba amesema adhabu hiyo imetolewa baada ya mamlaka hiyo kupima ubora wa huduma za mawasiliano katika robo ya mwisho ya mwaka 2020 na kubaini kuwa watoa huduma hao hawakufikia baadhi ya vigezo vya viwango vya ubora.