Hayo ameyasema leo wakati wa ziara ya kukagua miradi ya upanuzi wa huduma ya maji inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) inayohusisha ujenzi wa matenki na upanuzi wa mtandao.
Miradi hiyo itanufaisha Manispaa za Kinondoni na Ubungo na Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo ukiwa unahusisha matenki matano yenye ujazo wa Lita Milioni 6.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhandisi Kalobelo amesema mradi huu ulio mbioni kukamilika umeanza kuonesha manufaa kwa wananchi wa Changanyikeni kuanza kupata maji.
Mhandisi Kalobelo amesema, matarajio ya serikali ni kuona wananchi wanapata maji safi na salama na maji ni rasilimali adimu wananchi wanatakuwa watunze miundo mbinu.
Amesema, kulikuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi wa Goba, Wazo, Changanyikeni na Salasala ya kukosa maji kwa muda mrefu ila kumalizika kwa miradi hii mikubwa iliyowezeshwa na serikali kupitia Wizara ya Maji wananchi wataanza kunufaika baada ya kuyasubiri maji kwa muda mrefu.
" mradi huu ni wa awamu ya kwanza, kuna mradi wa pili ambao serikali tayari imepata hela kutoka Benki ya Dunia utakaowanufaisha wananchi walio maeneo ambayo hajayanufaika na mradi kwa kwanza," amesema Mhandisi.
Amewapongeza DAWASA kwa jitihada wanazozionyesha kwa kuhakikisha wananchi wanapata maji na ametoa rai kwa wananchi wajiunge kwenye mradi huu ili wapate maji safi na salama.