Benki ya NBC yaing’arisha Kariakoo Derby  

01May 2022
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM
Nipashe Jumapili
Benki ya NBC yaing’arisha Kariakoo Derby  

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara , NBC Premiere League jana iliipamba mechi ya watani wa jadi katika soka la Tanzania kati ya Yanga na Simba kwa kukabidhi tuzo na zawadi kwa mchezaji bora  na kocha bora wa mwezi Machi katika ligi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara, NBC Premiere League Theobald Sabi (Kushoto) akikabidhi hundi yenye thamani ya sh mil 1 kwa mchezaji wa klabu ya Simba Clatous Chama alietangazwa mchezi bora wa ligi hiyo kwa mwezi Machi. (Picha kulia) akikabidhi hundi yenye thamani ya sh mil 1 kwa kocha wa klabu ya Simba Pablo Franco alietangazwa kocha bora wa ligi hiyo kwa mwezi Machi wakati wa mechi kati ya Simba na Yanga iliyofanyika kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam jana. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi ndiye aliyeongoza shughuli hizo kwa kukabidhi  tuzo na zawadi ya fedha kiasi cha Sh. mil 1, kwa mchezaji wa Simba SC, Clatous Chama alietangazwa mchezi  bora wa ligi hiyo kwa mwezi Machi sambamba na Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Pablo Franco ambae alitangazwa kocha bora kwa mwezi huo na hivyo kuzawadiwa tuzo pamoja na fedha kiasi cha Sh. milioni 1 kutoka kwa mdhamini huyo.
 

Tukio hilo lililoshuhudiwa na maelfu ya mashabiki waliojitokeza kutazama mechi hiyo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, lilitanguliwa na matukio mengine mengi ikiwemo mapokezi ya wateja wa benki hiyo kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini  walioshinda katika Droo ya Jaza Kibubu Na NBC.

Washindi hao walipata fursa ya kushuhudia mechi hiyo wakiwa wamelipiwa gharama zote  ikiwemo za usafiri, malazi sambamba na kukatiwa tiketi za VIP kwa ajili ya kushuhudia mtanange huo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana.

Pamoja na washindi hao benki hiyo pia iliandaa mwaliko rasmi kwa ajili ya wateja wake mashuhuri wakiwemo viongozi waandamizi kutoka mashirika na taasisi mbalimbali pamoja na wadau wengine wa benki hiyo waliopata wasaa kupata chakula cha mchana pamoja na viongozi wa benki hiyo kisha kwa pamoja walielekea Uwanja wa Taifa kushudia mechi hiyo wakiwa katika msafara maalum.

Aidha, mashabiki waliojitokeza kutazama mechi hiyo walipata fursa ya kupata huduma mbalimbali za kifedha kutoka benki ya NBC kupitia maofisa wake mbalimbali waliokuwa wakitoa huduma hizo kwenye viunga vya vya uwanja huo, hatua iliyotoa fursa kwa mamia ya mashabiki hao kujiunga na huduma za benki hiyo ikiwemo kufungua akaunti mbalimbali pamoja na kufanya mihamala ya kifedha wakiwa maeneo hayo.

Mashabiki waliojitokeza kutazama mechi hiyo walipata fursa ya kupata huduma mbalimbali za kifedha kutoka benki ya NBC kupitia maofisa wake mbalimbali waliokuwa wakitoa huduma hizo kwenye viunga vya vya uwanja huo, hatua iliyotoa fursa kwa mamia ya mashabiki hao kujiunga na huduma za benki hiyo ikiwemo kufungua akaunti mbalimbali pamoja na kufanya mihamala ya kifedha wakiwa maeneo hayo.

Msafara uliowabeba viongozi wa benki ya NBC pamoja na wadau mbalimbali wa benki hiyo ukifika Uwanja wa Taifa wa Benjamin Mkapa kushudia mechi hiyo.