SportPesa ambao ni wadhamini wa timu za Simba, Yanga na Singida United, walikabidhi vifaa hivyo jana kwa
Meneja wa timu ya Bunge, John Kadutu kwenye ofisi za Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Kadutu alisema SportPesa wamekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza michezo nchini na wanapaswa kupongezwa kwa hilo.
"Tunaamini kwa msaada huu wa vifaa utatuwezesha si tu kupendeza, lakini pia kufanya vizuri kwenye michuano hii inayoanza kesho," alisema Kadutu.
Aidha, kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Uwendeshaji wa Kampuni hiyo, Tarimba Abass, alisema kuwa Kampuni yake inaona fahari kuisaidia timu hiyo ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba anaamini timu hiyo itafanya vizuri katika mashindano hayo yanayofanyika nchini.
Vifaa vilivyokabidhiwa kwa timu hiyo ni pamoja na jezi, mipira, 'tracksuit' na vifaa vingine vya michezo kwa timu za mpira wa miguu, netiboli, riadha na mpira wa wavu.
Michuano hiyo inayoanza leo, inafanyika katika viwanja vya Uhuru, Uwanja wa Taifa, pamoja na Uwanja wa JK Park, huku ikitarajiwa kumalizika Desemba 11, mwaka huu.
Katika hatua nyingine kampuni hiyo leo inatarajiwa kuukabidhi Uwanja wa Taifa kwa Serikali baada ya kukamilika ukarabati wake.