NDANI YA NIPASHE JUMAPILI

Mshindi wa kwanza wa Bodaboda katika Kampeni ya Mastabata – Kotekote ya Benki ya NMB, Asumwisye Mwajeka (wapili Kushoto) akiijaribu pikipiki baada ya kukabidhiwa katika benki ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa.
Kushoto ni Meneja mwandamizi wa Idara ya Biashara za Kadi, Manfredy Kayala, kulia ni Meneja wa Benki ya NMB tawi la Mkwawa, Happiness Pimma na wapili kulia ni Kaimu Meneja wa Kanda ya Nyanda za juu, Manyilizu Masanja.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako (kushoto) akizungumza na watumishi na waajiri kutoka maeneo mbali mbali jijini Dar es salaam waliojitokeza kushiriki michezo katika bonanza la waajiri (Waajiri Health Bonanza) lililoandaliwa na Chama cha Waajiri nchini (ATE) nakufanyika katika viwanja vya Leaders Club.