Kimya cha viongozi Simba hakina afya kwa mashabiki
WANACHAMA na mashabiki wa Simba wanapitia katika wakati mgumu kutokana na timu yao kutofanya vizuri kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, hivyo kuelekea kuukosa ubingwa huo kwa msimu wa tatu mfululizo.