Usimamizi makini unatakiwa utoaji mikopo ya halmashauri
SERIKALI jana ilitangaza kuanza utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuanzia Julai, mwaka huu, kwa kutumia utaratibu mpya wa kupitia benki. Katika kuanza utaratibu huo mpya wa mikopo, mamlaka 10 za serikali za mitaa zitaanza kama maeneo ya majaribio.