Live updates

Rais Samia apokea Ripoti ya CAG na Taarifa ya Utendaji kazi ya TAKUKURU 2022/2023

Frank Monyo
Mwandishi
Picha ya kusanifiwa ya Rais Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba baada ya kupokea Ripoti ya CAG na Taarifa ya Utendaji kazi ya TAKUKURU 2022/2023 (Kushoto juu) Mkurugenzi TAKUKURU CP Salum Rashid Hamduni, chini CAG Charles Kichere.
Picha: Nipashe Digital, IKULU
Picha ya kusanifiwa ya Rais Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba baada ya kupokea Ripoti ya CAG na Taarifa ya Utendaji kazi ya TAKUKURU 2022/2023 (Kushoto juu) Mkurugenzi TAKUKURU CP Salum Rashid Hamduni, chini CAG Charles Kichere.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/2023 pamoja na taarifa ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa mwaka 2022/2023 leo Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 28 Machi, 2024.

Akiwasilisha Taarifa ya Utendaji kazi wa TAKUKURU, Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, CP Salum Rashid Hamduni, amesema taasisi hiyo katika operesheni mbalimbali za kiuchunguzi imefanikiwa kuokoa bilioni 87.59 na uokoaji huo ulihusisha uokoaji wa dola za kimarekani milioni 33 sawa na shilingi bilioni 36.34

Kupitia uchunguzi wa mkongo wa taifa ambao ulibainika kuwa Umoja wa Watoa Huduma za Mawasiliono ulijenga miundombinu ya mawasiliano kinyeme na makubaliano na hivyo kuikosesha serikali mapato kutokana na huduma zao kutopita katika mkongo wa taifa.

ATCL yapata hasara bilioni 56

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: ATCL
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Charles Kichere, amesema mashirika ya Umma yanayojiendesha kibiashara yamepata hasara. Mwaka 2022/23, ATCL imepata hasara ya Tsh. Bilioni 56.64, sawa na ongezeko la 61% kutoka hasara ya Mwaka 2021/22 iliyokuwa Tsh. Bilioni 35.24. Ikumbukwe kuwa Shirika hili lilipokea ruzuku ya Tsh. Bilioni 31.55 kutoka Serikalini.


MSD ilitoa zabuni ya ununuzi vifaa vya COVID 19 kinyume na matakwa

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: IKULU
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Charles Kichere.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Charles Kichere, amesema ukaguzi umebaini MSD ilitoa zabuni ya ununuzi wa vifaa vya maabara ambavyo ni vipimo vya COVID 19 kwa kampuni ambayo haikuwa mtengenezaji wa vifaa hivyo kinyume na makatwa ya zabuni, pia ilinunua vifaa hivyo bila kufuata ushauri, baada ya kufika kwa vifaa hivyo wataalamu walibaini havifai kwa matumizi yetu na tayari MSD ilikuwa imelipa fedha zote.

TAKUKURU yabaini ongezeko ujenzi wa vituo vya mafuta katikati ya makazi ya watu

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: IKULU
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), CP Salum Rashid Hamduni akiwasilisha ripoti mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), CP Salum Rashid Hamduni amesema walibaini Ongezeko la maombi ya Ubadilishwaji wa Matumizi ya Ardhi kutoka Matumizi ya awali na kuwa Matumizi ya Vituo vya Mafuta, huku tatizo la Ujenzi wa Vituo vya Mafuta katikati ya Makazi ya Watu likiongezeka na kuleta Changamoto ya Usalama wa Watu waishio karibu

Asilimia 20 ya vituo vya mafuta havikuwa na leseni ya ujenzi

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: TAKUKURU
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), CP Salum Rashid Hamduni.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), CP Salum Rashid Hamduni amesema asilimia 79 ya Vituo vilivyochambuliwa vilizingatia Sheria kwa kuwa na vibali vya ujenzi kutoka halmashauri ambapo ujenzi umefanyika, asilimia 21 ya vituo havikuwa na leseni wakati zoezi la ufuatiliaji linafanyika.




TAKUKURU yafanya uchambuzi mfumo ujenzi vituo vya mafuta 38 Dar, Pwani

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Kituo cha mafuta.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), CP Salum Rashid Hamduni, amesema walifanya uchambuzi kuhusu Mfumo wa Uzingatiaji wa taratibu za Ujenzi wa Vituo vya Mafuta katika Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani ambapo Vituo 38 vilihusika.

Watoa huduma za mawasiliano walipa dola milioni 20

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: IKULU
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU, CP Salum Rashid Hamduni.

Kupitia mkataba wa makubaliano kati ya umoja wa watoa huduma za mawasiliono na wizara ya habari mawasiliono na teknolojia umoja huo ulikubali kulipa dola za kimarekani milioni 20 taslimu katika kipindi cha miaka mitano pamoja na riba ya asilimia 3.5.