CCM imeonesha ukomavu kwa miaka 48 ya uhai wake
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) jana kiliadhimisha miaka 48 tangu kuanzishwa mwaka 1977. Chama hicho kilianzishwa baada ya kuunganishwa TANU, chama kilichopigania na kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara) na Afro Shiraz Party (ASP) kilichopigania na kufanikisha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar mwaka 1964.