Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda,akizungumza na Nipashe Digital hili Leo kwa njia simu amesema ajali hiyo imetokea Leo saa 10:30 alfajiri katika kijiji cha Malendi kilichopo kata ya Mgongo wilayani humo.
IDADI ya watu waliokufa katika ajali ya basi la Lujiga Express lenye namba za usajili T 315 CXX iliyotokea wilayani Iramba mkoani Singida imefikia 9 na majeruhi 19.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Daniel Paul. amesema kati ya majeruhi hao , watatu ambao walikuwa wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Iramba (Kiomboi) alikuwepo mwanamke mjamzito ambaye amefanyiwa operesheni na mtoto kukutwa amefariki tumboni.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED