Simbachawene ainyooshea kidole Ardhi

By Mary Mosha , Nipashe
Published at 03:01 PM Jun 12 2024
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimen-ti   ya   Utumishi   wa   Umma   na   Utawala   Bora, George Simbachawene.
Picha: Mary Mosha
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimen-ti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimen-ti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene ameaigiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya utafiti na kuishauri serikali ili kuondoa migogoro ya ardhi nchini kutokana na kuwasababishia wa-nanchi maumivu makubwa.

Simbachawene alitoa  agizo  hilo  jana  wakati  akifungua  mafunzo ya wachunguzi wasaid-izi  na  wachunguzi  wakuu  420  wa  TAKUKURU  katika  Shule  ya  Polisi Moshi (TPS).

Alisema utafiti unaonyesha migogoro   ya   ardhi   inatengen-ezwa      na   baadhi   ya   watumi-shi   wasio   waadilifu   hali   inay-opelekea    viongozi    kuwekeza    nguvu  nyingi  katika  utatuzi  wa  migogoro    badala  ya  kufikiria  maendeleo.

“Sekta  hii   imeleta   migogoro   mikubwa   sana,   imesumbua   familia  inaitesa  jamii,  kila  mkoa,  kila  wilaya,  kila  kata,  kijiji  pana  mgogoro  wa  ardhi,  inadumaza  maendeleo,  inaharibu  malengo  ya baadhi ya watu.Umempa     kiwanja     B,  una-shangaa   kiwanja   hicho   hicho   amepewa  C  na  F  na  wote  wana  hati    hivi    tunashindwaje    kuwatafuta  hao  wote  waliohusika  na kufanya hayo, kokote walipo waje   wajibu?   TAKUKURU   isaidieni   serikali   hatutaki   kusikia   tena  migogoro  hiyo,”  alisema  na  kuongeza kuwa:

“Kwa   sasa   Waziri   wa   Ardhi,   Nyumba     na     Maendeleo     ya     Makazi    ( Jerry    Silaa)    anapita    huku  na  huko  kuhakikisha  anatatua,  lakini  anakutana  na  watu  wamegushi  nyaraka  nyingi  sana  zinazopelekea   migogoro.

 Tuna   mifumo,  lakini  unakuta  kiwanja  kimoja  kina  michoro  miwili  na  hati mbili, hii haikubaliki. Shiriki-aneni na Jeshi la Polisi,  Tume ya Maadili  katika  kuweka  mkakati  wa kutokomeza jambo hili.

”Simbachawene  aliwata-ka    kuongeza  nguvu  kwenye  maeneo ya kutolea huduma ili  kukabiliana  na  tatizo  kubwa  lililopo katika eneo hilo.

“Wapo wenzetu wengine kuse-ma ukweli  wamegeuza maeneo hayo    kuwa  ni  sehemu  yao  ya  kupata  kiinua  mgongo  na  uta-jiri,” alisema.

Akizungumza  kuhusu  waajiriwa  wapya,   Simbachawene,       alisema   licha   kupitia   kwenye   mchakato  mbalimbali  wa  upati-kanaji  wa  ajira,  bado  kuna  mti-hani  wa  mwisho  wa  kuwahakik-ishia uhalali huo.

“Mchakato  ulikuwa  ni  mkubwa,  waombaji  walikuwa  20,000  waliotakiwa ni 420, kuingia kwenye  kundi  hilo  sio  jambo  dogo,  lakini   kama   nilivyosema   safari   bado ndefu, katika miezi mitano ya  mafunzo    ndipo  mtakapojihakikishia uhakika wa ajira hii.

“Nyinyi  ni  wasomi  wa  taalu-ma  mbalimbali  na  mna  uwezo  mkubwa ,   kumbukeni   mnaokwenda    kuwafanyia    uchunguzi    huo  nao  ni  wasomi  kama  nyinyi  mkipambana    kutoa    elimu    na    wao    wanapambana    kuharibu    ila   shabaha   ya   serikali   ni   kuhakikisha inajenga     chombo     cha wanataaluma ambacho kita-fanya utafiti, kitazuia kwa mbinu mbalimbali mtakazofundishwa,” alisema Simbachawene.

Alisema  chombo  hicho  kinahitaji    watumishi  waadilifu  na  wazalendo,  wenye  nidhamu  ya  kutosha    ili  kuleta  taswira  ra-hisi  na  kuongeza  kuwa  kazi  yao  itakuwa kutoa taarifa kwa mamlaka  ikiwa kuna eneo lolote linaonekana kuwa na dosari.

“TAKUKURU   ijikite   zaidi   ka-tika  kuzuia  na  sio  kupambana,  unapofikia   kupambana   unaku-wa   tayari   umechelewa,   hivyo   ongezeni viherehere mpaka mtu hela  ikiingia  leo  aseme  moyoni,  bora  nikajenge  tu  darasa,  kituo  cha   afya   vionekane   ili   niache   kufuatwa fuatwa na TAKUKURU, msipofanya hivyo watu wanaan-za    mipango    mara    anapoona    fedha.”

Awali,  Mkurugenzi  Mkuu  wa  TAKUKURU,  Kamishna  wa  Polisi, Salimu Hamduni, alisema kwa kipindi  cha  miaka  mitatu,  seri-kali  imeipatia  taasisi  hiyo  kibali  cha  kuajiri  watumishi  1,190  na  watumishi  wa  kubadili  kada  102  ambao walijiendeleza.

Alisema wanafunzi wa mafunzo      ya   uchunguzi   (wajunguzi   wakuu   310)   waliwasili   shuleni   hapo  Mei  31,  mwaka  huu  na  wa-natarajiwa   kukaa   chuoni   hapo   kwa  ajili  ya  kuanza  mafunzo  ya  miezi mitano.

“Mafunzo      yanatarajiwa   kufanyika    kwa    nadharia    na    vitendo.    Wiki    tisa        watafanya    kwa  vitendo,  kila  mwajiriwa  wa  TAKUKURU   atapaswa   atambue   ya ajira yake itategemea uadilifu  na nidhamu kwa muda wote wa maisha wake,” alisema.

Mkuu  wa  Mkoa  wa  Kilimanjaro,     Nurdin     Babu,     alisema     TAKUKURU    ni    jicho        litakalochangia maendeleo na kuwataka wataalamu kutumia fursa  ili kuongeza tija kwa taifa.