NDANI YA NIPASHE LEO

Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mette Norgaard Dissing-Spandet (kushoto) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala (kulia) wakibadilishana nyaraka za makubaliano baada ya tukio la kutiliana saini mkataba wa ruzuku ya nyongeza kiasi cha shilingi za kitanzania 5.6 bilioni (USD 2.4 million) zilizotolewa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Denmark (DANIDA) kwa ajili ya kutekeleza mradi wa upatikanaji wa haki nchini kwa kipindi cha mwaka mmoja kati ya Januari na Desemba 2021, unaotekelezwa na LSF.