Wanafunzi wa Shule ya Wasichana ya Kipok iliyopo wilayani Monduli mkoani Arusha wameaswa kutokubali kishika uchumba wangali wakiwa wanaendelea na masomo.
Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Dawati la Jinsia na watoto Wilaya ya Monduli Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Jacqueline Uhwelo jana mchana wakati wa kikao kilichofanyika shuleni hapo kati ya Dawati hilo na wanafunzi hao wa kidato cha kwanza hadi cha Nne wapatao 1,000.
Alisema kwamba, kumekuwa na tabia ya baadhi ya makabila kupeleka kishika uchumba kama vile Pete kwa wazazi wa wanafunzi wa kike huku wakitarajia wafunge nao ndoa mara tu baada ya kumaliza shule
Alisema hali hiyo inafifisha ndoto za wasichana hao ambao pengine wanawaza kusonga mbele kimasomo.
"Matukio hayo yanawaathiri sana baadhi ya wanafunzi ambao wengine wanapata ujauzito hata kabla ya kumaliza kidato cha Nne lakini pia kitendo hicho pia kinasababisha mwanafunzi ahamishe mawazo yake toka kwenye masomo na kufikiria kuolewa". Alifafanua mkuu huyo wa Dawati.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED