KUNDI la waasi wa mrengo wa shoto nchini Colombia la National Liberation Army (ELN), limetangaza kuwa litaondoa tangazo lake la awali la kusitisha kwa muda vitendo vyake vya utekaji nyara.
Kundi hilo limesema linachukua hatua hiyo kwa sababu serikali ya Colombia imeshindwa kutimiza makubaliano yaliyofikiwa wakati wa mazungumzo ya amani.
Mojawapo ya makubaliano hayo ni kuundwa kwa mfuko wa fedha utakaofadhili mchakato wa kusaka amani na kuwezesha kundi la ELV kuweka chini silaha. Hata hivyo kundi hilo limesema ahadi hiyo ya serikali haijatimizwa.
Upande wa serikali ya Colombia umesema mfuko huo haujaanzishwa kwa sababu kundi hilo liliomba duru nyingine ya mazungumzo.
Tangazo la ELV linaloashiria kuanza tena kwa vitendo vyake vya utekaji nyara, litaleta changamoto mpya kwenye mazungumzo kati ya pande hizo mbili yaliokuwa yameanza tangu mwishoni mwa mwaka 2022.
DW
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED