Elimu ya malipo mtandao ihusishe wananchi wote
WAZIRI wa Fedha, Dk,. Mwigulu nchemba, Alhamisi wiki hii, aliwasilisha mapendekezo ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka 2024/25 jijini Dodoma. Katika mapendekezo hayo, serikali imepanga kutumia Sh. trilioni 49.35 kwa ajili ya matumizi ya kawaida kwa shughuli za serikali na miradi ya maendeleo.