MWENYEKITI wa UVCCM Mkoa wa Kagera Faris Burhani amewataka vijana mkoani humo hususani maofisa usafirishaji maarufu kama bodaboda kuendelea kuwa wavumilivu wakati serikali inaendelea na maboresho ya sera ya mikopo ya vijana, wanawake na watu mwenye ulemavu.
Mikopo hiyo ilisitishwa na serikali kutokana na baadhi ya vikundi kukopa fedha bila kurejesha kwa Wakati sambamba na udanganyifu katika utolewaji wa mikopo hiyo.
Burhani ametoa rai hiyo wakati akiongea na wananchi pamoja na bodaboda wa Kata ya Kabindi Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera katika ziara yake ya kikazi ya siku 16 iliyoanza Aprili 14 katika Wilaya hiyo.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED