Waamuzi wachezeshe kwa haki kuelekea kumaliza msimu wa ligi
WAKATI Ligi Kuu Bara ikiwa imebakisha raundi tano tu kutamatika, bado kuna uchezeshaji usioridhisha kwa baadhi ya waamuzi. Kwa bahati mbaya sana uchezeshaji huo unaangukia kwa timu zinazosaka ubingwa, huku zile zinazotafuta nafasi ya nne ili zicheze mechi za kimataifa mwakani, au zinazokimbia kushuka daraja, zikionekana kukandamizwa zaidi.