Haya yakitekelezwa kikamilifu sekta ya elimu italeta mageuzi
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, jana aliwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25 wenye vipaumbele vitano. Katika utekelezaji wa vipaumbele hivyo, vyenye lengo la kuimarisha ubora wa elimu nchini, Waziri Mkenda aliomba Bunge kupitisha Sh. trilioni 1.96.